Upinzani "Washinda" urais Ivory Coast
Tume ya uchaguzi wa Ivory Coast imesema mgombea urais wa upinzani Alassane Ouattara ameshinda uchaguzi wa raundi ya pili ya urais, ingawa mahakama ya katiba imepinga matokeo hayo.

Alassane Ouattara
Mwandishi wa BBC John James aliyepo mjini Abidjan amesema kutakuwa na mvutano kati ya taaisisi hizo mbili huku matokeo yake yakiwa hayajulikani.
Wafuasi wa rais Laurent Gbagbo walijaribu kupinga matokeo hayo, wakisema kumekuwa na wizi upande wa kaskazini.
Eneo hilo bado limesalia chini ya udhibiti wa waasi wa zamani, anao ambalo Bw Ouattara ana umaarufu mkubwa. Soma habari kamili
0 comments:
Post a Comment