AIBU BOSI WA BANDARI AFUMWA AKILA URODA

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter


Na Mwandishi Wetu
Ofisa Mwandamizi Uchukuzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Makao Makuu jijini Dar, Kitengo cha Makontena, Peter Milanzi (54) amejikuta ndani ya aibu nzito kufuatia madai kwamba, amekutwa akiwa na mke wa mtu kwenye nyumba ya kulala wageni ‘gesti hausi’, Ijumaa Wikienda linashuka na ‘diteilzi’. 

Tukio hilo lililoacha historia, lilijiri Desemba Mosi, 2010 (Siku ya Ukimwi Duniani) majira ya alasiri kwenye chumba namba tano cha hoteli moja (jina tunalo), Buguruni, Dar.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, mume aliyejitambulisha kwa jina la Shaha Juma alidai kumbamba Milanzi akiwa na mkewe wa ndoa aitwaye Salia.

Chanzo hicho kikaongeza kudai kuwa, kabla ya fumanizi hilo lililokusanya mashuhuda kibao, mume wa mwanamke huyo alikuwa na kibarua kizito cha kufuatilia nyendo za ‘wezi’ hao mpaka ndani ya chumba hicho. Endelea kusoma habari hii...

0 comments: